Tuesday 3 May 2016

Mtangazaji wa Clouds amtaja Adam mchomvu akilaumu Redio nyingine.


Mtangazaji wa Clouds FM, Diva amesema
nyimbo zake pamoja na za mtangazaji
mwenzake, Adam Mchomvu zinabaniwa na redio yingine, kitu ambacho anaona si sawa.

Amesema redio za mikoani ndizo zimekuwa
zikiwapa support bila kujali kuwa wanatoka
Clouds lakini redio karibu zote za Dar zimekuwa zikibania nyimbo zao.

Diva ambaye anaandaa album yake, The Life of The Diva, amesema kuwa hicho ni kitu ambacho angependa kuona kinafutika.

Mimi naona wako so unprofessional, mbona sisi Clouds FM watu wazuri, Sam Misago kaja, katoa wimbo ataitwa kwenye XXL nyimbo yake itachezwa, sisi mbona nyimbo zetu hamchezi?” amehoji Diva.

Diva anaendelea kusema “Nilipeleka nyimbo East Africa Radio na ina haki zote za kuchezwa na haikuchezwa kwasababu natoka Clouds Media, kwanini wanatufanyia hivi? Hii ni biashara, wao wafanye kazi zao, na sisi tufanye kazi zetu lakini when it comes to music, sisi tunafanya serious kabisa"

Chanzo: Bongo5

No comments: