Thursday 28 April 2016

Majengo 20 ya CCM Kubomolewa Moshi.


Ubomoaji wa majengo yaliyojengwa kinyume na sheria za mipango miji katika Manispaa ya Moshi unatarajiwa kuanza hivi karibuni.

Ubomoaji huo unakusudiwa kuambatana
na uvunjaji wa majengo zaidi ya 20 ya
Chama cha Mapinduzi (CCM) yaliyopo katika Kata ya Mawenzi.

Meya wa manispaa hiyo, Raymond Mboya
amewaambia waandishi wa habari kuwa wanatarajia kusimamia ipasavyo sheria hiyo ili kuhakikisha majengo yaliyojengwa kinyume na sheria yanavunjwa.

Mboya amesema sheria ni lazima ifuatwe
haijalishi ni chama gani kimejenga kinyume.

Leo tunapata ugumu wa kuwa jiji kutokana na sisi wenyewe kushindwa kusimamia sheria za mipango miji, hatuwatendei haki wakazi wa Manispaa ya Moshi ni lazima ifike wakati watu
tujue kuna mamlaka ambayo imekabidhiwa kusimamia mji,”amesema Mboya.

Kwa upande wake Loth Ole Mesele, Katibu wa CCM wilaya ya Moshi mjini amesema hajapata taarifa hizo za kubomolewa kwa majengo ya chama hicho.

Magufuli amsimamisha kazi kisa hachukui mshahara.


Rais Magufuli ametengua uteuzi wa
Mkurugenzi Mtendaji TIC, Bi Juliet Kaoruki ambapo pamoja na mambo mengine sababu ya Mh Rais. Kutengua uteuzi huo ni kutokana na kutochukua mshahara wa serikali.

Kadhalika Bi. Kairuki ameingia kwenye list ya watumishi kadhaa wa serikali waliosimamishwa kazi na kupewa ahadi ya kupangiwa kazi nyingine.

Kivuli cha taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo  April,28 2016


Wednesday 27 April 2016

Uhaba wa umeme wasababisha watumishi wa umma kufanya kazi siku kwa wiki Venezuela.



Serikali ya Venezuela imeagiza wafanyakazi
wake wawe wakifanya kazi siku mbili kwa wiki.Hii ni hatua ya muda iliyochukuliwa kutokana na uhaba wa umeme.

Makamu wa Rais Aristobulo Isturiz ametangaza kwamba watumishi wa umma wanafaa kufika kazini Jumatatu na Jumanne pekee hadi mzozo wa sasa wa nishati umalizike.

Venezuela imekabiliwa na ukame mkubwa ambao umepunguza maji kwenye bwawa lake kuu la kufulia umeme.



Lakini upinzani umeituhumu serikali kwa
kutodhibiti vyema mzozo wa sasa. Agizo la kupunguzwa kwa siku za kufanya kazi,
lililotolewa kupitia runinga ya taifa na Bw Isturiz.

"Hakutafanywa kazi katika sekta ya umma
Jumatano, Alhamisi na Ijumaa, ila tu majukumu muhimu sana.” alisema.

Amesema Venezuela imeathiriwa sana na hali ya hewa ya El Nino na kwamba hali ya kawaida itarejea baada ya mvua kuanza kunyesha.

Serikali imekuwa ikichukua hatua kadhaa
kupunguza matumizi ya umeme. Februari, maduka yaliagizwa kupunguza muda
ambao yanafunguliwa kila siku na pia kujaribu kujizalishia umeme.

Mapema wiki hii, serikali pia ilisongeza mbele saa kwa nusu saa ili kupunguza mahitaji ya umeme kwa ajili ya mwanga mapema jioni.

New Song: Barnaba - Wanifaa.(MP3)



DOWNLOAD HERE

Tuesday 26 April 2016

New audio: Nuh Mziwanda Ft Ally Kiba - Chupa Jike



                  DOWNLOAD HERE

Mke Wa rais mstaafu wa Kenya afariki dunia Jumanne hii


FirstLady wa zamani wa Kenya Lucy Kibaki amefariki dunia Leo Jumanne.

Taarifa ya Rais Uhuru Kenyatta imedai kuwa Mrs Kibaki alifariki akitibiwa katika hospitali ya Bupa Cromwell ya London.

“Her excellency has been unwell for the last one month and has been receiving treatment here in Kenya and subsequently in the United Kingdom,” yamesema maelezo hayo.

Mrs Kibaki alikuwa amelazwa kwenye hospitali ya Nairobi mwezi uliopita baada ya kutafuta matibabu katika hospitali ya Gertrude ya Muthaiga.

Ameacha watoto wanne, Judy Wanjiku, Jimmy Kibaki, David Kagai na Tony Githinji.

Watatu wakamatwa wakisafirisha Madawa Kilimanjaro


Watu watatu akiwemo mmoja raia wa Kenya
wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro baada ya kukamatwa na madawa
ya kulevya aina ya Mirungi na Bangi kilo 54
na misokoto ya Bangi 4,500 ikisafirishwa
kutoka nchini Kenya kwenda mkoani Arusha.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro
Bw.Wilbrod Mutafungwa amesema
watuhumiwa hao wamekamatwa katika
maeneo ya njia panda Himo wilaya ya Moshi
na Sanya juu wilaya ya Siha wakiwa wameficha madawa hayo ya kulevya kwenye
miili yao kuanzia maeneo ya tumboni hadi
miguuni.

Amewataja waliokamatwa ni Vitalis Victor
mfanyabiashara mkoani Arusha, Naftal Mvoyi
mkazi wa Voi nchini Kenya, Maulid Maulis
mkazi wa Arusha ambao walikuwa
wakisafirisha Mirungi kilo 44 kwa kutumia
magazeti na gundi ya karatasi na kisha
kuifunika kwenye nguo walizokuwa wamevaa
wakitokea nchini Kenya kuelekea jiji la
Arusha.

Ripota wetu amefanikiwa kuzungumza na
baadhi ya vijana wanaojihusisha na matumizi
ya madawa ya kulevya katika manispaa ya
Moshi na kueleza kwamba changamoto
kubwa inayowabaili ni ukosefu wa ajira hali
inayowasababisha baadhi yao kujihusisha na
matukio ya uhalifu.

Matumizi ya madawa ya kulevya yameathiri
vijana wengi kiafya kutokana na baadhi yao
kushindwa kufanya shughuli za maendeleo na
hivyo kulazimika kujihusisha na matukio ya
wizi katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

MJ record yavunja mzizi wa Fitna Video ya Sugu- Freedom


Mr Blue analalamika kuwa Sugu ameupora
wimbo wake ‘Freedom’ aliokuwa amemshirikisha kwa kutoa verse zake na kuufanyia video iliyotoka jana.

Lakini katika kila malalamiko, ni vyema kusikiliza pande zote zinazohusika kwenye jambo husika ili kuupata ukweli. MJ Records walioutayarisha wimbo huo wamezungumza kuelezea mambo yalikuwaje.

Producer mkuu wa studio hiyo, Marco Chali
ameuambia mtandao mmoja kuwa beat ya wimbo huo ilitengenezwa na mdogo wake, Daxo Chali aliyetengeneza chorus yake na alimpa msanii wake Lizzy aliyeingiza.

“Ngoma ilikuwa ipo tayari na ilikuwa inasubiria verse tu kadhaa halafu ilikuwa ni ngoma yake [Daxo]. Kwahiyo jamaa [Blue] akawa ameipenda tukampa akasema atamshirikisha Mr Two,” amesema Marco.
Walipoifanya, Blue aliiamua kuiachia kupitia
Mkito peke yake kwa maana kwamba hakuiachia ngoma rasmi. Anasema baada ya muda Sugu alimpigia simu kumuomba kuwa afanye version nyingine ya wimbo huo na aifanyie kabisa na video.

Anadai alimuambia Sugu aongee na Daxo
waliyekubali kuufanya tena hadi video ikafanyika huku yeye [Marco] akiwa hajui chochote kilichoendelea baada ya hapo. Na Marco anasema pia hakuhusika kwenye uingizaji wa sauti zote mbili zaidi ya kuzifanyia mixing peke yake.

Marco amesema anadhani wawili hao [Sugu na Blue] waliongea kuhusu hatua hiyo na kwamba wao kama studio hawakuwa na kipingamizi chochote kuhusu kurudiwa kwa wimbo huo kwasababu walitaka wimbo ufike mahali.

Hata hivyo Marco amedai kuwa wote wawili [Sugu na Blue] hawakulipia wimbo huo na
kwamba MJ Records iliwapa kwasababu ya ‘love’ tu. Marco anasema anashangaa kuona Mr Blue sasa hivi anatoa malalamiko hayo.

“Ni kwasababu mimi nilipenda tu kutoa studio
bure kwanini usijitahidi ukapeleka hiyo nyimbo ikafika sehemu ikafahamika, at least pia akili za watu zilizotumika watu wazione. Na ndio hicho kitu naona ni kizuri, yeye kwa mfano angefanya hata video, sidhani kama Sugu angerudia huo wimbo,” ameongeza Marco.

“Na yeye aliposema kwamba anataka afanye
video, namaanisha kwamba walishaongea na
Blue kwamba yeye afanye video. Halafu Daxo
wasije kumweka tena kwenye matatizo
akaonekana kwamba ni producer mzinguaji ni
vitu ambavyo havitamsababishia biashara na dogo mwenyewe ndio anataka kutoka. Na anajua wazi kuwa ni watu wazima wameongea kule,” amesisitiza Marco.

Naye Sugu amedaiwa kujibu malalamiko ya Blue kwa ujumbe huo chini kwenye WhatsApp.

Chanzo: Bongo5

Sugu Ndani ya tuhuma za wizi wa wimbo.


Msanii Mr blue kupita account yake ya Instagram amelalama akieleza mashambulizi yake kwa mbunge Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu au Mister II baada ya Sugu kuachia video ya wimbo unaokwenda kama "Freedom"

Mr Blue ameandika alifanya wimbo huo na Sugu ila ameshangazwa na kitendo cha Mbunge huyo kuondoa Verse yake na kuingiza mengine mwenyewe bila kumpatia Taarifa.


BongoHomeTz imejaribu kumtafuta Joseph Mbilinyi kwa Simu yake ya mkononi bila mafanikio.

Mbunge Joseph Mbilinyi A.K.A Sugu ametoa video ya wimbo mpya. Sugu-Freedom (Official video)


Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi (Sugu) baada ya kimya kirefu katika kazi yake ya awali ya Music sasa ameachia Video ya wimbo wake mpya unaoenda kwa jina la "Freedom".

Tazama video ya Sugu hapa.Imeongozwa na Hanscana


            

Wednesday 20 April 2016

Donald Trump na Hillary Clinton Watambiana kwa kura.


Zaidi ya nusu ya kura zilizohesabiwa katika
uchaguzi wa awali wa vyama katika
kinyang’anyoro cha urais nchini Marekani katika mji wa New york, zinaonesha kwamba Donald Trump na Hillary Clinton wamepata ushindi mkubwa zaidi.

Hillary Clinton ambaye amemshinda mpinzani
wake Bernie Sanders kwa ushindi mkubwa
ameeleza katika hotuba yake kuwa ushindi wa
chama chake cha Democratic umeweza
kuwaunganisha zaidi wapinzani wake kuwa
wamoja.

Hata hivyo New York inatajwa kuwa ngome
nyingine ya Donald Trump,ambapo Cruz yeye
hesabu za kura zake zimeonekana kugoma
mapema kabisa katika chama chake cha Republican.

Wakati Hillary Clinton amemshinda mpinzani
wake Bernie Sanders kwa ushindi mkubwa,
amewaambia wapinzani wake kuwa kuna la
ziada linalowafanya wawe wamoja zaidi ya
kuwagawa.

Source: BBC NEWS

Mrembo Naj avikwa pete ya Ahadi na Barakah Da Prince




Barakah Da Prince ambaye kwa sasa amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na msanii wa kike, Naj, amedai kupiga hatua zaidi kuelekea
kwenye uchumba.

Amefunguka kuhusu
uhusiano wao alipokuwa akizungumza na moja ya mitandao mikubwa nchini Tanzania uitwao Bongo5.


Yeah ni kweli mimi na Naj tuna uhusino na hadi kwetu nimeshamtambulisha na yeye kwao najulikana na pia nimemvisha pia pete, sio ya uchumba ila ni Promise Ring,” amesema
Barakah.

Kuhusu kufanya kazi Barakah amesema “kuna kazi pia ambazo tumefanya ila hazitatoka sasa hivi hadi kwanza kila mtu atoe single yake halafu ndio itakuja hiyo ngoma ya pamoja mimi na Naj,”



Naj Amethibitisha kwa kusema
"Ni kweli Barakah amenivisha pete kama
alivyosema. Kwangu ni furaha sana maana
nimeshakuwa na mahusiano yaliyopita lakini
sikuwahi kufanya kitu kama hiki. Naona kabisa kuwa mahusino haya ni ya ukweli na naona kuna malengo kabisa, nafurahia kwakweli.”

Na kuongeza “Bado hatujaanza kuishi wote ila muda mwingi tupo pamoja, nafurahia mahusiano yangu ya sasa"

Saturday 16 April 2016

T.I.D Amenyoosha Maelezo. Juma Nature asema Magufuli atosha.



Baada ya KR kujitambulisha kuwa yeye ndiye Rais wa RADA Entertainment na Juma Nature kumpinga kwa kejeli akisema hamtambui Rais yoyote zaidi ya Rais Magufuli hatimaye TID anyoosha maelezo.

T.I.D amesema muda ukifika watamuapisha rasmi KR Mulla kuwa Rais wa Radar Entertainment na kutoa sababu za kufanya kazi na KR Mulla katika label yake.

Zaidi eNews ilipotaka kupata maelezo ya kina juu ya tuhuma za TID kuhusishwa na matumizi ya madawa ya kulevya, TID aligoma kusema chochote, na hata alipoulizwa juu ya tuhuma hizo kwa wasanii wengine pia TID alisema “Muda ukifika nitaongea nyie endeleeni kuongea vitu msivyovijua”.

Wednesday 13 April 2016

Olamide ameweka wazi kumkubali msanii huyu.


Boss wa YBNL , Olamide, Hakika amekuwa akitambua na kukubali kazi nzuri inayofanywa na yeyote akisikia na kuona kipaji na sasa amemkubali mwimbaji Simi.

Simi’s Ni msanii Chipkizi nchini Nigeria ambae amekuwa amefanikiwa kumkuna Olamide kwa audio na video zake nzuri anazozitoa.

 “Simi is too talented!.” aliema Olamide, ambapo tayari msanii Sami tayari ameshajiunga na lebo ya Oscar Music Production ambayo inasimamiwa na
producer na mwandishi wa mashairi mwenye kipaji, Oscar Heman Ackah.

Diamond Platnumz: Heri niwe na Kijiji cha Nyumba Tandale kuliko ninunue nyuma Marekani.


Msanii Diamond Platnumz amefunguka
kuhusu suala la yeye kutonunua nyumba nchini Marekani kama wasanii wenzake wakubwa wa Afrika wanavyofanya.

Diamonda amefunguka hilo kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na kusema kuwa haoni umuhimu wa yeye kununua nyumba Marekani, tofauti na alivyonunua Afrika Kusini, kwani kule ilimlazimu.

Pia Diamond aliweka wazi kuwa kununua nyumba Marekani kwake hakuna faida, ni heri awe na kijiji cha nyumba Tandale au Mwananyamala, lakini si Marekani.


Nna nyumba South Africa kwa sababu nina familia South Africa kwa hiyo ni lazima ninunue nyumba south Africa, lakini sina sababu ya kusema
ninunue nyumba Marekani, ninunue nyumba Marekani kwa sababu gani, kwanza sipapendi",
alisema Diamond.

Friday 8 April 2016

Meneja Wa Diamondi na TipTop Connection Ajibu Tuhuma zinazomkabili.

Meneja wa Diamond na Tip Top Connection.

Babu Tale amefunguka na kuzungumzia madai ya kuwa huwa anawabania baadhi ya wasanii wa nje ya management yake ili kuwapa nafasi wasanii wake.

Akizungumza katika kipindi cha The Playlist cha Times FM, Babu Tale amesema wale ambao wanasema kwamba wanabaniwa, wameshindwa kukiamini kile wanachokifanya ndio maana hawafanikiwi.

“Ukiwa na mentality kwamba Tale ndio anaendesha watu, mimi nilishawahi kukwambia piga ngoma hii,” Tale alimuuliza mtangazaji.

“Mimi sina radio wala TV. Unajua kila mtu ana mtanzamo wake, Ni kweli kuna watu wanasema mimi nimetawala muziki ni kweli, kwa sababu ngoma za wasanii wangu nilizotoa hivi karibuni ni kali, mimi kila siku nawaza media inataka kulipa kupiga ngoma, media haiwezi kulipa ngoma mbaya, kwa hiyo mimi nafikiria kesho,”

“Sijawahi kuwasimamia Weusi, lakini wanafanya vizuri kwenye muziki, mimi simsimamii Ommy Dimpoz na anafanya vizuri, ana jiamini na anafanya kazi yake katika ubora. Wapo pia ambao mimi nawasimamia na hawafanyi vizuri, kwa sababu hawajiamini na hawafanyi kazi nzuri.

Nipo kwenye team ambayo ina njaa na mimi mwenyewe nina njaa, sitaki kufanya kazi yangu tu ilimradi, wakati natoa nyimbo kama namtoa underground, hata kama natoa nyimbo ya Diamond naangaika kama namtoa ya underground,” aliongeza Tale.

Meneja Wa Mr Flevour apata mtoto miezi mnne tu tangu kuoa.

Mr Flavour
Meneja wa Msanii kutoka Nigeria Mr. Flavour bwana Benjamin Omesite na mkewe Ifeyinwa jana walibahatika kupata mtoto.Benjamin Omesite na mkewe Ifeyinwa walipata mtoto wa kike. Ikumbukwe wawili hawa walioana Mwezi Januari mwaka huu.


X-Girlfriend wa Wizkid ameshare picha za Arusi Yake.

Sophie Rammal

Sophie Rammal  Ameshare baadhi ya Picha za ndoa yake. 

Sophie Rammal ambae ni mpenzi wa zamani wa msanii Wizkid kutoka Nigeria amepost picha hizo akiwa katika mapozi tofauti na Mume wake anaejulikana kama Wale Alakija. Ndoa yao ilifungwa mwezi Januari Huko Lagos. 

Sophie Rammal Amekuwa akitrend sana kutokana na kushirikiana mambo mengi ikiwemo katika ”Holla at your Boy Music” Sophie na Wizkid waliDate kwa kipindi kifupi tu na kuachana. 

Tazama Picha Zaidi, 





Thursday 7 April 2016

Tanzia: Aliekuwa mbunge Viti maalumu Afariki Dunia


Dada ya Tundulisu na aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA), Mhe. Christina Lissu Mughwai amefariki dunia muda mfupi uliopita
katika hospitali ya Aga Khan Dar.

Marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa cancer tangu mwaka jana.

Picha ya Diamond akiwa amevaa Hereni puani haimaanishi ametoboa pua.

Picha ya Diamond Platnumz ikimuanyesha akiwa na Hereni puani. (Picha na Mtandao)
Kwa saa kadhaa zimeenea taarifa za mwimbaji staa wa bongofleva Diamond Platnumz kuonekana katoboa pua, hii habari imepewa nguvu kutokana na picha aliyoipost Diamond mwenyewe kwenye Instagram akionekana katoboa pua.

Ukweli ni kwamba Diamond hajatoboa pua kama wengi walivyodhani ambapo
Meneja wake aitwae Sallam aliwajibu hivi mashabiki. "Usiamini kila unachoona kwenye picha au unachoambiwa, mklikuwa mmelala sana amewaamsha kidogo


Maneno ya Meneja Sallam yanamaanisha kwamba sio kweli Diamond katoboa pua, ni mchezo tu na baada ya hiyo picha ya kutoboa pua Diamond aliweka picha nyingine inayoonekana hapa chini akiwa fresh kabisa.



Chanzo: Millard Ayo

Tommy Thomass: Mashabiki Mjiandae Mambo mazuri yanakuja



Msanii wa Hip Hop  kutokea mkoani Kilimanjaro Tommy Thomas amesema kitu kipya kitatoka Ndani ya mwezi huu.

Tommy Thomas akizungumza na BongoHomeTz amesema kwa sasa yupo katika hatua za mwisho ili aweze kuachia kibao hicho kipya.

"Kwa sasa nafanya makubaliano ya kibiashara na baadhi ya kampuni, ikiwemo Mkito na BongoHomeTz pia Cover na mambo mengine yanaelekea kukamilika. Hivyo Nadhani week ijayo nitatoa wimbo rasmi" Alisema Tommy Thomas.

Tommy Thomas aliitonya BongoHomeTz kuwa ngoma mpya inayokuja inaitwa "naongea" amemshirikisha becka title wa b.o b. Micharazo. studio ni Frezzo rec chin ya producer aidan machord

Kadhalika Aliongeza kuwa mara tu baada ya kutoa wimbo huo atakuwa na Media Tour katika media mbalimbali hapa nchini na hata nje ya nchi.

Pamoja na hayo Thommy Thomas ametumia fursa hii kuwaomba mashabiki wake wakae mkao wa kula. Kwa sasa Tommy Thomas Anatamba na Kibao alichomshirikisha Walter Chilambo kinachofahamika kama "Twende". Bofya hapa kudownload moja ya nyimbo kali za Tommy Thomas. (Tommy Thomas Ft Walter Chilambo-Twende MP3)

Sunday 3 April 2016

Mubba_C atua Singida kutambulisha nyimbo mpya.



Mkali wa Mistari kutoka Singida anaefanyia harakati zake Jijini Arusha Mubba_C amefanya ziara ndani ya Mkoa wa Singida kwa ajili ya kutambulisha kazi zake mpya.

Mubba_C ameiambia BongoHomeTz kuwa atatumia kituo cha redio cha Standard Redio kilichopo Mkoani Singida ili kufikisha kazi zake kwa maelfu ya mashabiki wake mkoani humo.

Wiki iliyopita Mubba_C alikuwa ndani ya jiji la Arusha akifanya utambulisho wa kazi zake mpya ambapo alihitimisha kwa kuzungumza Na mashabiki wake kupitia kipindi cha The Beat Show cha Arusha One FM radio.

Tayari ameshatambulisha nyimbo mpya ambazo zimepokelewa vizuri zikiwemo wimbo Nieleze, Hasoling Mapenzi kikohozi,Walisema na Wa Pekee

Hata Hivyo Mubba_C amewaomba mashabiki wake waendelee kumpa sapoti kwa kuomba nyimbo zake kwenye vituo vya redio Na pia wahudhurie matamasha pale watakaposikia kuwa Mubba C anahusika.

NEW SONG| T.I.D ft Dully Sykes X Joh Makini - Confidence



                  DOWNLOAD HERE

New Song| Nikki Mbishi Ft Becka Title_Kwanini Mimi [Audio]



                         DOWNLOAD HERE