George Masaju, Mwanasheria Mkuu wa Serikali |
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju amesema Miswada ya marekebisho ya Sheria ipo jikoni ambapo mabadiliko hayo yataisaidia serikali kutimiza ahadi zake.
Kadhalika Masaju amesema mswada wa sheria ya kuanzisha Mahakama Maalumu ya Mafisadi uko tayari na utawasilishwa Aprili mwaka huu bungeni, kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa kuwa sheria, kutoa nafasi kwa mahakama hiyo kuanza kazi.
Ikumbukwe kuwapo kwa mahakama ya mafisadi ni ahadi ya mh. Rais John Pombe Magufuli aliyoitoa alipokuwa akijinadi katika kampeni za uchaguzi mkuu uliofanyika Mwaka jana Oct 25.
Chanzo: EATV
No comments:
Post a Comment