Sunday 28 February 2016

Masaju: Muswada wa sheria ya kuanzishwa mahakama ya mafisadi umekamilika

George Masaju, Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju amesema Miswada ya marekebisho ya Sheria ipo jikoni ambapo mabadiliko hayo yataisaidia serikali kutimiza ahadi  zake.

Kadhalika Masaju amesema mswada wa sheria ya kuanzisha Mahakama Maalumu ya Mafisadi uko tayari na utawasilishwa Aprili mwaka huu bungeni, kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa kuwa sheria, kutoa nafasi kwa mahakama hiyo kuanza kazi.

Ikumbukwe kuwapo kwa mahakama ya mafisadi ni ahadi ya mh. Rais John Pombe Magufuli aliyoitoa alipokuwa akijinadi katika kampeni za uchaguzi mkuu uliofanyika Mwaka jana Oct 25.

Chanzo: EATV

No comments: