Tuesday 23 February 2016

Penzi la Wema kwa Idrisa mashakani. Wema amechukua Uhamuzi huu

Penzi donda ndugu, ndio msemo pekee unaoweza kuupachika katika kipindi kama hiki cha migogoro ya mahusiano.
Japo hatujafahamu hasa chanzo ni nini, na nini hasa kimetokea lakini dalili za awali tu zinaonesha penzi kati ya muigizaji Wema Sepetu na mshindi wa Big Brother Idriss Sultan limefika kikomo.
Vita ya maneno kati ya wawili hawa, iliibukia mitandaoni huku kila mmoja akirusha vijembe kwa mwenzake.
Katika hali ambayo haikutarajiwa na wengi, mastaa hawa wamelivunja penzi lao mapema mno, huku mwanadada Wema Sepetu akionekana muhanga zaidi kwani amefuta picha zote za Idriss alizowahi kupost mtandaoni Instagram.
Matatizo kati yao yameanza kuibuka tangu siku ilipowekwa wazi kuwa, Ujauzito wa Wema umeharibika.

No comments: