Wednesday 13 April 2016

Diamond Platnumz: Heri niwe na Kijiji cha Nyumba Tandale kuliko ninunue nyuma Marekani.


Msanii Diamond Platnumz amefunguka
kuhusu suala la yeye kutonunua nyumba nchini Marekani kama wasanii wenzake wakubwa wa Afrika wanavyofanya.

Diamonda amefunguka hilo kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na kusema kuwa haoni umuhimu wa yeye kununua nyumba Marekani, tofauti na alivyonunua Afrika Kusini, kwani kule ilimlazimu.

Pia Diamond aliweka wazi kuwa kununua nyumba Marekani kwake hakuna faida, ni heri awe na kijiji cha nyumba Tandale au Mwananyamala, lakini si Marekani.


Nna nyumba South Africa kwa sababu nina familia South Africa kwa hiyo ni lazima ninunue nyumba south Africa, lakini sina sababu ya kusema
ninunue nyumba Marekani, ninunue nyumba Marekani kwa sababu gani, kwanza sipapendi",
alisema Diamond.

No comments: