Sunday 3 April 2016

Mubba_C atua Singida kutambulisha nyimbo mpya.



Mkali wa Mistari kutoka Singida anaefanyia harakati zake Jijini Arusha Mubba_C amefanya ziara ndani ya Mkoa wa Singida kwa ajili ya kutambulisha kazi zake mpya.

Mubba_C ameiambia BongoHomeTz kuwa atatumia kituo cha redio cha Standard Redio kilichopo Mkoani Singida ili kufikisha kazi zake kwa maelfu ya mashabiki wake mkoani humo.

Wiki iliyopita Mubba_C alikuwa ndani ya jiji la Arusha akifanya utambulisho wa kazi zake mpya ambapo alihitimisha kwa kuzungumza Na mashabiki wake kupitia kipindi cha The Beat Show cha Arusha One FM radio.

Tayari ameshatambulisha nyimbo mpya ambazo zimepokelewa vizuri zikiwemo wimbo Nieleze, Hasoling Mapenzi kikohozi,Walisema na Wa Pekee

Hata Hivyo Mubba_C amewaomba mashabiki wake waendelee kumpa sapoti kwa kuomba nyimbo zake kwenye vituo vya redio Na pia wahudhurie matamasha pale watakaposikia kuwa Mubba C anahusika.

No comments: