Wednesday 20 April 2016

Mrembo Naj avikwa pete ya Ahadi na Barakah Da Prince




Barakah Da Prince ambaye kwa sasa amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na msanii wa kike, Naj, amedai kupiga hatua zaidi kuelekea
kwenye uchumba.

Amefunguka kuhusu
uhusiano wao alipokuwa akizungumza na moja ya mitandao mikubwa nchini Tanzania uitwao Bongo5.


Yeah ni kweli mimi na Naj tuna uhusino na hadi kwetu nimeshamtambulisha na yeye kwao najulikana na pia nimemvisha pia pete, sio ya uchumba ila ni Promise Ring,” amesema
Barakah.

Kuhusu kufanya kazi Barakah amesema “kuna kazi pia ambazo tumefanya ila hazitatoka sasa hivi hadi kwanza kila mtu atoe single yake halafu ndio itakuja hiyo ngoma ya pamoja mimi na Naj,”



Naj Amethibitisha kwa kusema
"Ni kweli Barakah amenivisha pete kama
alivyosema. Kwangu ni furaha sana maana
nimeshakuwa na mahusiano yaliyopita lakini
sikuwahi kufanya kitu kama hiki. Naona kabisa kuwa mahusino haya ni ya ukweli na naona kuna malengo kabisa, nafurahia kwakweli.”

Na kuongeza “Bado hatujaanza kuishi wote ila muda mwingi tupo pamoja, nafurahia mahusiano yangu ya sasa"

No comments: