Picha ya Diamond Platnumz ikimuanyesha akiwa na Hereni puani. (Picha na Mtandao) |
Kwa saa kadhaa zimeenea taarifa za mwimbaji staa wa bongofleva Diamond Platnumz kuonekana katoboa pua, hii habari imepewa nguvu kutokana na picha aliyoipost Diamond mwenyewe kwenye Instagram akionekana katoboa pua.
Ukweli ni kwamba Diamond hajatoboa pua kama wengi walivyodhani ambapo
Meneja wake aitwae Sallam aliwajibu hivi mashabiki. "Usiamini kila unachoona kwenye picha au unachoambiwa, mklikuwa mmelala sana amewaamsha kidogo"
Maneno ya Meneja Sallam yanamaanisha kwamba sio kweli Diamond katoboa pua, ni mchezo tu na baada ya hiyo picha ya kutoboa pua Diamond aliweka picha nyingine inayoonekana hapa chini akiwa fresh kabisa.
Chanzo: Millard Ayo
No comments:
Post a Comment