Saturday 16 April 2016

T.I.D Amenyoosha Maelezo. Juma Nature asema Magufuli atosha.



Baada ya KR kujitambulisha kuwa yeye ndiye Rais wa RADA Entertainment na Juma Nature kumpinga kwa kejeli akisema hamtambui Rais yoyote zaidi ya Rais Magufuli hatimaye TID anyoosha maelezo.

T.I.D amesema muda ukifika watamuapisha rasmi KR Mulla kuwa Rais wa Radar Entertainment na kutoa sababu za kufanya kazi na KR Mulla katika label yake.

Zaidi eNews ilipotaka kupata maelezo ya kina juu ya tuhuma za TID kuhusishwa na matumizi ya madawa ya kulevya, TID aligoma kusema chochote, na hata alipoulizwa juu ya tuhuma hizo kwa wasanii wengine pia TID alisema “Muda ukifika nitaongea nyie endeleeni kuongea vitu msivyovijua”.

No comments: