Thursday 7 April 2016

Tommy Thomass: Mashabiki Mjiandae Mambo mazuri yanakuja



Msanii wa Hip Hop  kutokea mkoani Kilimanjaro Tommy Thomas amesema kitu kipya kitatoka Ndani ya mwezi huu.

Tommy Thomas akizungumza na BongoHomeTz amesema kwa sasa yupo katika hatua za mwisho ili aweze kuachia kibao hicho kipya.

"Kwa sasa nafanya makubaliano ya kibiashara na baadhi ya kampuni, ikiwemo Mkito na BongoHomeTz pia Cover na mambo mengine yanaelekea kukamilika. Hivyo Nadhani week ijayo nitatoa wimbo rasmi" Alisema Tommy Thomas.

Tommy Thomas aliitonya BongoHomeTz kuwa ngoma mpya inayokuja inaitwa "naongea" amemshirikisha becka title wa b.o b. Micharazo. studio ni Frezzo rec chin ya producer aidan machord

Kadhalika Aliongeza kuwa mara tu baada ya kutoa wimbo huo atakuwa na Media Tour katika media mbalimbali hapa nchini na hata nje ya nchi.

Pamoja na hayo Thommy Thomas ametumia fursa hii kuwaomba mashabiki wake wakae mkao wa kula. Kwa sasa Tommy Thomas Anatamba na Kibao alichomshirikisha Walter Chilambo kinachofahamika kama "Twende". Bofya hapa kudownload moja ya nyimbo kali za Tommy Thomas. (Tommy Thomas Ft Walter Chilambo-Twende MP3)

No comments: