Wednesday 20 April 2016

Donald Trump na Hillary Clinton Watambiana kwa kura.


Zaidi ya nusu ya kura zilizohesabiwa katika
uchaguzi wa awali wa vyama katika
kinyang’anyoro cha urais nchini Marekani katika mji wa New york, zinaonesha kwamba Donald Trump na Hillary Clinton wamepata ushindi mkubwa zaidi.

Hillary Clinton ambaye amemshinda mpinzani
wake Bernie Sanders kwa ushindi mkubwa
ameeleza katika hotuba yake kuwa ushindi wa
chama chake cha Democratic umeweza
kuwaunganisha zaidi wapinzani wake kuwa
wamoja.

Hata hivyo New York inatajwa kuwa ngome
nyingine ya Donald Trump,ambapo Cruz yeye
hesabu za kura zake zimeonekana kugoma
mapema kabisa katika chama chake cha Republican.

Wakati Hillary Clinton amemshinda mpinzani
wake Bernie Sanders kwa ushindi mkubwa,
amewaambia wapinzani wake kuwa kuna la
ziada linalowafanya wawe wamoja zaidi ya
kuwagawa.

Source: BBC NEWS

No comments: