Ommy Dimpozz kwa poz Tanzania Musician |
Akizungumza na kipindi cha Friday Night Live,kinachoruka kupitia EATV, Ommy Dimpoz alisema mwaka huu atamtambulisha msanii mmoja kutoka lebo ya PKP kwa kirefu Poz Kwa Poz
“Baada ya kuanzisha lebo yangu ya PKP, Mwaka huu kumtambulisha msanii wangu mmoja. Najua watu watasema kuwa mpaka fulani aanzishe na wewe ndio uige,Ila nilitangaza muda kuwa nimeanzisha lebo yangu.” Alisema Dimpozz
Ommy Dimpoz kwa sasa anatamba na kibao chake cha Achia Body ambacho kwa sasa kina walau takribani miezi mitatu ivi.