Sunday 27 March 2016

Taarifa ya Chad kujiondoa #2017AFCON na Majibu wa mustakabali wa timu zilizosalia.


Taarifa za  timu ya Taifa ya Chad kujitoa kwenye mashindano ya AFCON zimekuja saa chache kabla ya kuvaana na Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars.

Mfano wa barua iliyobainisha Chad Kujitoa katika michuano ya #AFCON2017 (Picha na YerickoNyerere)


Baada ya kujitoa kwa timu hiyo sasa zitatumika kanuni za michuano hiyo zinazosimamiwa na CAF. Na huu ndio ufafanuzi wa hatma wa timu zilizopo kwenye kundi moja na Chad.

Kwa mujibu wa Kanuni sasa Matokeo yote ya Chad yamefutwa na hayatahusishwa na timu yoyote hata kama timu hiyo iliwahi kuifunga Chad na kujinyakulia pointi au kuwa katika nafasi iliyopo kutokana na magoli iliyoifunga Chad.

Kadhalika kundi litatoa mshindi mmoja ambae anashika nafasi ya juu zaidi kwenye kundi tofauti na makundi mengine yatatoa timu mbili za juu katika kundi.

Tweet kadhaa za CAF wakilitolea ufafanu sakata hilo la kujitoa kwa timu ya  Chad


Ikumbukwe Chad ilikuwa katika kundi G na Nigeria, Misri (Egypt) na Tanzania, Taifa Stars.

No comments: